Historia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaanzia April 26 mwaka 1964
siku ambayo Nchi ya Jamuhuri ya Tanganyika ambayo kwa sasa ni Tanzania
bara pamoja na iliyokuwa Jamuhuri ya Zanzibar (inayojumuisha Visiwa vya
Pemba na Unguja) ziliungana na kuwa nchi moja.
Kumbu kumbu zinaonyesha Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar ziliingia mkataba tarehe 22 Aprili 1964 huko Zanzibar kwa lengo
la kuunganisha nchi hizo mbili baada ya kutiwa saini na viongozi wa
nchi hizo kwa wakati huo ambao ni aliyekuwa Rais wa Tanganyika, Hayati
Mwalimu Julius Nyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar,
Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.
Baada ya kutiwa saini kwa mkataba huo au kama unavyojulikana hati ya
Muungao baadae makataba huo ulipelekwa kwenye mabunge yote mawili yaani
Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi tarehe 26 Aprili, 1964 ili
uridhiwe rasmi kuwa sheria ya Muungano ambapo nchi mpya inayojulikana
“Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar” ilizaliwa ambapo sherehe
kubwa zilizofana za kuchanganya udongo wa pande zote mbili zilifanyika
ili ku.
Hata hivyo nchi hii mpya iliendelea kujulikana kwa jina hilo
la”Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar” hadi Oktoba 28, 1964
lilibadilishwa rasmi kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jina
linatumika hadi hivi leo kupitia Sheria ya Jamhuri ya Muungano, Sheria
namba 61 ya mwaka 1964.
Kwa ujumla Muungano huo wa kuunganisha nchi mbili kwa hiari umekuwa
ukisifiwa kwamba ni Muungano wa kipekee barani Afrika Professa
Paramagamba Kabudi Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yeye anasema
katika utafiti wake amegundua ni Muungano huo ndio pekee wa hiari
uliodumu hadi hivi leo.
Muundo wa Muungano uliokubaliwa
Nchi mpya iliyozaliwa yaani Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni
muungano wenye Muundo wa vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji
ambavyo ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Pia vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki ambavyo ni
Mahakama ya Jamhuri ya Muungano na Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar;
na pia vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia
utekelezaji wa shughuli za umma ambavyo ni Bunge la Jamuhuri ya Muungano
na Baraza la Wawakilishi.
Katika utekelezaji wa shughuli zake Serikali ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania yenyewe imepewa mamlaka ya kushughulikia mambo yote ya
Muungano kama yalivyoainishwa katika Katiba ya Tanzania na mambo yale
yasiyo ya Muungano kwa upande wa Tanzania Bara huku Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar yenyewe imepewa mamlaka ya kushughulikia mambo
yote yasiyo ya Muungano kwa upande wa Tanzania Zanzibar.
Mambo ya Muungano
Mambo ya Muungano ya kwanza kabisa yaliyoanishwa kwenye Katiba ya muda ya mwaka 1965 yalikuwa ni 11 ambayo ni
• Katiba na Serikali ya Muungano
• Mambo ya Nchi za Nje
• Ulinzi
• Polisi
• Mamlaka juu ya mambo yanohusika na hali ya hatari
• Uraia
• Uhamiaji
• Mikopo na Biashara ya Nchi za Nje
• Utumishi katka Serikali ya Jamhuri ya Muungano
• Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika,
ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa
nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
• Bandari mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na
simu.
Hata hivyo Baadae Mambo ya Muungano yaliongezeka kutoka kumi na moja (11) hadi ishirini na mbili (22)
Likiwemo suala la sarafu na benki kuu ambapo nchi zote zilianza kutumia sarafu moja hadi hivi leo.
Mbali na mafanikio yaliyopatikana Muungano huu wa Tanganyika na
Zanzibar umekuwa ukipitia safari ya mabonde na malima ambapo wapo
wanaona kuwa umewapa manufaa huku wengine wakidhani muungano hauna
faida.
Kwa sasa Tanzania ipo kwenye mchakato wa kuandika Katiba Mpya ambapo
suala la Muundo upi wa Muungano unaofaa kati ya Muundo uliopendekezwa
kwenye rasimu ya Katiba wa serikali tatu na muundo wa sasa unaopigiwa
debe na chama tawala wa serikali mbili ni mjadala uliopamba moto katika
nchi hii.
Hata hivyo kwa vyovyote vile pamoja na changamoto na matatizo yote hayo ni wazi muungano huo kufikisha miaka 50 sio jambo dogo.